Dodoma FM

Diwani ahimiza wananchi kuzingatia lishe bora Ndachi

24 December 2025, 3:47 pm

Diwani wa Kata Mnadani, Mugendi Karenge akiongea na wakazi wa Ndachi.Picha na Anwary Shaban.

Maadhimisho hayo yaliambatana na utoaji wa elimu ya lishe, ushauri wa afya, pamoja na upimaji wa afya kwa watoto.

Na Anwary Shaban.
Diwani wa Kata Mnadani, Mugendi Karenge amewataka wananchi wa Mtaa wa Ndachi kuzingatia masuala ya afya na lishe bora ili kujenga jamii yenye nguvu na ustawi endelevu.

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Afya na Lishe yaliyofanyika katika mtaa huo.

Sauti ya Mugendi Karenge

Kwa upande wake Muuguzi Kituo cha Afya Chang’ombe, Nyemo Mussa amesema ni muhimu mzazi kumpeleka mtoto kliniki kupata chanjo ya magonjwa kama vile pepopunda.

Sauti ya Nyemo Mussa .

Kwa Upande wao wananchi wamesema kuwa elimu hiyo walipewa kwa kujifunza wataitumia ipasavyo na wale wazazi ambao wapo nyumbani watakwenda kuwapa elimu ya lishe.

Sauti za wananchi.