Dodoma FM

Mahudhurio hafifu mkutano wa mtaa mwenyekiti avunja kikao

18 December 2025, 4:10 pm

Licha ya matangazo kutangazwa mataani lakini idadi ya watu walio fika hawampi kibali Cha kuendelea na mkutano huo.Picha na ccm blog.

Mkutano ulioitishwa ulikuwa na ajenda muhimu kama vile ardhi hivyo ni vigumu kuendesha ajenda hizo muhimu na kuchangia na mawazo ya watu wachache.

Na Victor Chigwada.

Wananchi wa mtaa wa Ihumwa A wametakiwa kuhudhuria mikutano ya mtaa ili kushiriki maamuzi ya maendeleo ya mtaa pamoja.

Hayo yana jiri baada ya mwenyekiti wa mtaa  wa Ihumwa A kulazimika kuahirisha kikao cha mtaa kutokana na idadi ndogo ya watu walio fika kwenye mkutano huo.

Lameki Mbinda mwenyekiti wa mtaa huo amesema kuwa licha ya matangazo kutangazwa mataani lakini idadi ya watu walio fika hawampi kibali Cha kuendelea na mkutano huo.

Mbinda amewatia moyo wale walio fika na kuwataka wakawe wajumbe wema Kwa wengine  ili wawahimize kufika  kwenye mkutano mwingine utakapo tangazwa.

Sauti ya Lameki Mbinda.

Mbinda ameongeza kuwa mkutano ulioitishwa ulikuwa na ajenda muhimu kama vile ardhi hivyo ni vigumu kuendesha ajenda hizo muhimu na kuchangia na mawazo ya watu wachache .

Sauti ya Lameki Mbinda.

Nao baadhi ya wananchi walio fika katika mkutano huo wametoa wito Kwa jamii kubadilika na kufika katika mikutano kwani maendeleo ya mtaa yanategemea uwepo wa uhusiano mzuri wa jamii na viongozi wake.

Sauti za wananchi