Dodoma FM

Wananchi wahimizwa kutunza mazingira

15 December 2025, 3:51 pm

Utunzaji bora wa mazingira unasaidia pia kulinda rasilimali za nchi.Picha na Mtandao.

Utunzaji wa mazingira ni muhimu katika jamii hususani utunzaji wa milima.

Na Farashuu Abdallah.

Wananchi wamehimizwa kutunza mazingira ili kuepuka athari hasi zinazoweza kutokea katika jamii.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa kitengo cha mawasiliano Serikalini halmashauri ya jiji la Dodoma Dennis Gondwe wakati akizungumza na Dodoma Fm amesema utunzaji wa mazingira ni muhimu katika jamii hususani utunzaji wa milima kwani ni chanzo kimojawapo cha kukuza uchumi wa nchi.

Aidha, Gondwe  amemaliza kwa kuishauri jamii juu ya utunzaji wa mazingira ili kulinda rasilimali zilizopo.

Sauti utunzaji wa mazingira.