Dodoma FM

Wananchi watakiwa kuchangamkia fursa za serikali

28 November 2025, 2:18 pm

Picha ni Naibu waziri wa wizara ya maendeleo ya jamii,jinsia,wanawake na makundi maalumu Mhandisi .Maryprisca Mahundi katika kikao cha kuangazia fursa na vikundi vya malezi na matunzo ya watoto kata ya Ihumwa jijini Dodoma.Picha na Maendeleo ya jamii.

Ni vyema wananchi wakachangamkia fursa zinazotolewa na Serikali ikiwemo fursa ya mikopo kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

Na Mariam Matundu.
Wananchi wametakiwa kuchangamkia fursa zinazotolewa na Serikali kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

Wito huo umetolewa tarehe 27 Novemba na Naibu waziri wa wizara ya maendeleo ya jamii,jinsia,wanawake na makundi maalumu Mh.Mhandisi .Maryprisca Mahundi katika kikao cha kuangazia fursa na vikundi vya malezi na matunzo ya watoto kata ya Ihumwa jijini Dodoma.

Waziri Mahundi amesema ni vyema wananchi wakachangamkia fursa zinazotolewa na Serikali ikiwemo fursa ya mikopo kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

Picha ni vikundi vya malezi na matunzo ya watoto kata ya Ihumwa jijini Dodoma.Picha na Maendeleo ya jamii.Picha na Maendeleo ya jamii.
Sauti ya Mhandisi .Maryprisca Mahundi

Aidha Mh.Naibu Waziri amewasihi wazazi wawe na tabia ya kuwashirikisha watoto katika kazi za kiuchumi ili kujenga kizazi kizuri chenye uwajibikaji.

Sauti ya Mhandisi .Maryprisca Mahundi

Nao baadhi ya wanavikundi wameishukuru Serikali kwa kuwawezesha katika fursa mbalimbalina kuwapa elimu ya malezi bora kwa watoto.

Sauti za wanavikundi.