Dodoma FM

Hofu ya kukosa daraja yawakumba wakazi wa majeleko

23 October 2025, 4:06 pm

Kukosekana kwa daraja katika mto Kinyasungwi kumekuwa na atari kubwa hasa kwa wanafunzi wa eneo hilo.Picha na Dodoma fm.

Changamoto hiyo imekuwa ikiathiri shughuli za wananchi hao kutokana na maji hayo kudumu kwa muda bila ya kupungua.

Na Victor Chigwada.

Kuelekea katika msimu wa masika, wananchi wa kijiji cha Majeleko Wilayani Chamwino mkoani Dodoma wameonyesha kuwa na hofu kutokana na mto Kinyasungwi kujaa maji na kukata mawasiliano.

Changamoto hiyo imekuwa ikiathiri shughuli za wananchi hao kutokana na maji hayo kudumu kwa muda bila ya kupungua.

Sauti za wananchi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji Cha Majeleko Ndg.Charlesi Milangasi amesema kukosekana kwa daraja katika mto Kinyasungwi kumekuwa na atari kubwa hasa kwa wanafunzi kutokana na kulazimika kukaa nyumbani na kusubiri maji kupungua.

Sauti ya Charlesi Milangasi

Nao baadhi ya wanafunzi kutoka Kijiji jirani cha Chinangali wameeleza namna ambavyo huwaathiri kimasomo kutokana na mto huo kujaa maji.

Sauti za wanafunzi.