Dodoma FM

Kituo cha Afya Ilazo chaanza kutoa huduma za kibingwa

22 October 2025, 3:20 pm

Picha ni muonekano wa kituo cha Afya ilazo kilichopo kata ya Ipagala Jijini Dodoma .Picha na Lilian Leopold.

Huduma hizo za kibingwa zinatarajiwa kusaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali za rufaa, sambamba na kuinua kiwango cha utoaji wa huduma za afya katikajamii.

Na Lilian Leopold.
Wananchi Mtaa wa Ilazo na maeneo ya jirani Jijini Dodoma wametakiwa kutumia fursa kupata matibabu ya kibingwa yanayotolewa katika kituo cha afya Ilazo.

Wito huo umetolewa na Daktari kutoka Kituo cha Afya Ilazo, Stevene Adam Chikoti ambapo amesema kuwa huduma za kibingwa hizo zinahusisha tiba za magonjwa ya ndani, magonjwa ya akinamama, upasuaji na magonjwa ya watoto, hatua inayolenga kuboresha afya za wakazi wa eneo hilo.

Picha ni baadhi ya wakazi wa ilazo wakiwa wanapatiwa huduma kituoni hapo.Picha na Lilian Leopold.
Sauti ya Stevene Adam Chikoti.

Kwa upande wake, Hezron Kalinga,AfisaTabibuwaKituo cha Afya Ilazo, amesema utoaji wa huduma hizo umeanza ambapo hadi sasa wagonjwa 12 wa magonjwa ya ndani wamekwishahudumiwa.

Sauti ya Hezron Kalinga.