Dodoma FM

Ulaji wa mayai unavyoimarisha afya, lishe bora

10 October 2025, 3:16 pm

Leo dunia inaadhimisha Siku ya Yai Duniani, siku maalum inayotumika kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa yai katika kuboresha afya na lishe ya binadamu. Picha na Mtandao.

Kupitia siku hii, jamii inatakiwa kutambua umuhimu wa mayai, kwani kupitia ulaji wa mayai, familia zinaweza kupunguza utapiamlo na kuimarisha afya za watoto.

Na Anwary Shaban.

Siku hii, inayoadhimishwa kila mwaka mwezi Oktoba, inalenga kuongeza uelewa kuhusu nafasi ya yai katika kuboresha afya ya binadamu kutokana na protini, vitamini, na madini muhimu yaliyomo ndani yake.

Akifanya mahojiano na Taswira ya Habari Afisa Lishe kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Beatrice Moshi amesema yai husaidia ukuaji wa watoto, kuimarisha nguvu za watu wazima, na kulinda afya ya ubongo kwa rika zote.

Sauti ya Beatrice Moshi.

Aidha, Bi. Moshi ameongeza kuwa mayai yanapendekezwa zaidi kwa makundi maalum kama watoto wa umri wa miaka 6 na kuendelea, wanawake wajawazito, watu wenye udhaifu wa mwili, wazee, na wale walioko katika matibabu ya kurejesha afya.

Sauti ya Beatrice Moshi.

Kwa upande wao, wafanyabiashara wa mayai wamesema wanazingatia ubora wa bidhaa kuanzia kwa wauzaji wa jumla hadi kwa watumiaji wa mwisho.

Sauti za wafanyabiashara wa mayai.

Nao baadhi ya wananchi wamesema kuwa yai limekuwa sehemu ya mlo wa kila siku. Wameeleza faida zake ikiwa ni pamoja na kumjenga mtoto kiakili na kuongeza protini mwilini.

Sauti za wananchi.

Siku ya Yai Duniani ilianzishwa rasmi mwaka 1996 na Shirika la Kimataifa la Yai (International Egg Commission), na imeendelea kuwa jukwaa muhimu la kuelimisha jamii kuhusu faida za yai katika maisha ya binadamu.