Dodoma FM

Ukosefu wa umeme kilio kwa wakazi wa Ngh’ambaku

15 September 2025, 12:46 pm

Wakazi wa kijiji hicho wanalazimika kutumia mafuta ya dizeli kwaajili ya uendeshaji wa mashine hali inayopelekea mafuta hayo kuuzwa kwa gharama kubwa.Pacha na Habari leo.

Licha ya wananchi hao kutumia mafuta ya dizeli kukabiliana na changamoto ya umeme bado mafuta hayo hayakidhi mahitaji yao.

Na; Victor chigwada.
Imeelezwa kuwa matumizi ya mafuta ya Diesel Kwa wakazi wa Kijiji Cha Ngh’ambaku Wilaya ya Chamwino imekuwa ni changamoto kubwa Kwa wananchi kwani hayakidhi mahitaji zaidi ya kuwaumiza watumiaji.
Wamesema changamoto hiyo ya bei inachangiwa na matumizi ya mafuta katika mashine jambo ambalo linahitaji kutatuliwa Kwa kufungwa nishati ya umeme.

Sauti za wananchi.

Mwenyekiti wa Kijiji Cha Ngh’ambaku Bw.Juma Muyeya amesema kuwa wakazi wa Kijiji hicho wanakumbana na adha ya maji kwani kisima Chao kimatumia mfumo wa mafuta ya diesel.

Sauti ya Bw.Juma Muyeya.

Muyeyu ameongeza ni vyema Serikali kutatua changamoto hiyo Kwa kupeleka nishati ya umeme kwenye kisima Cha maji kwani tofauti na hivyo kisima hicho kinawaumiza wananchi hususani wafugaji.