Dodoma FM

Ajenda ya lishe shuleni iwe endelevu

21 August 2025, 4:09 pm

Picha ni mkuu wa wilaya ya Dodoma Alhaji Jabir Shekimweri pamoja na walimu wengine wakigawa uji kwa wanafunzi.Picha na Lilian Leopold.

Alhaj Jabir Shekimweri  amewasistiza walimu kuwa ajenda ya lishe shuleni iwe endelevu na kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanapata chakula.

Na Lilian Leopold.

Katika juhudi za kuboresha elimu na afya ya wanafunzi, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Alhaj Jabir Shekimweri, amesema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma inaendelea kutekeza agizo la Rais kuwa watoto ni kipaumbele cha kwanza kupata chakula wakiwa shuleni.

Ameyabainisha hayo mara baada ya kutembelea Shule ya Msingi Kizota, August 20,2025 kwa lengo la kukagua utekelezaji wa ajenda ya  lishe shuleni.

Sauti ya Alhaj Jabir Shekimweri.

Kwa upande wao Afisa lishe wa Jiji la Dodoma, Alfa Fanuel na Mwalimu Mkuu  Shule ya Msingi Kizota Hamida Mkingule wamesema kupitia utekelezaji wa  agenda ya lishe shuleni umesaidia kupunguza utoro  shuleni na kuwasaidia wanafunzi kushiriki kikamilifu katika masomo na michezo.

Sauti za Mwalimu na Afisa lishe.