Dodoma FM

PPRA yafungua mafunzo mfumo mpya wa NeST

20 August 2025, 5:59 pm

Picha ni washiriki mbalimbali pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa PPRA, Bw. Dennis Simba, wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku kumi kuhusu moduli mpya ya Usimamizi wa Mikataba katika Mfumo wa NeST, .Picha na PPRA.

Serikali kupitia PPRA imesema moduli hiyo mpya inalenga kuondoa changamoto zilizojitokeza awali na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa mikataba ya umma, ili kuhakikisha thamani ya fedha na uwajibikaji vinaimarika.

Na Seleman Kodima.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Denis Simba, amesema changamoto mbalimbali katika usimamizi wa mikataba ya umma zimekuwa zikisababisha upotevu wa rasilimali, kupungua kwa thamani ya fedha na kuzorota kwa huduma zinazotolewa kwa wananchi.

Akizungumza jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya moduli mpya ya usimamizi wa mikataba ndani ya mfumo wa NeST, Simba amesema changamoto hizo ni pamoja na ucheleweshwaji wa utekelezaji wa miradi, ukosefu wa ufuatiliaji wa karibu, mabadiliko ya vifungu vya mikataba bila kufuata taratibu, na malipo yasiyoendana na kazi zilizotekelezwa.

Sauti ya Denis Simba.

Mafunzo hayo yamejumuisha taasisi mbalimbali za ununuzi yamelenga kuwajengea uwezo watendaji kutumia moduli mpya ya mfumo wa NeST. Washiriki wamesema mfumo huo umeongeza usawa na uwazi katika mchakato wa kuomba na kusimamia tenda za serikali.