Dodoma FM

Vyama vya siasa vyatakiwa kufanya siasa za kistaarabu

19 August 2025, 3:13 pm

Picha ni MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi .Picha na Jamhuri Media.

Ikumbukwe kuwa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge na urais zitafanyika kuanzia Agosti 28 hadi Oktoba 28, siku inayofuata Jumatano, Oktoba 29, 2025 itakuwa siku ya upigaji kura.

Na Farashuu Abdallah.

Vyama vya siasa vimetakiwa kufanya siasa za kiusataarabu katika kipindi hiki cha kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa Octoba 2025.

Wito huo umetolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi kwenye mafunzo kuhusu sheria ya gharama za uchaguzi katika ukumbi wa JNICC  Mkoani Dar es salaam.

Jaji Mutungi amesema ni muhimu kwa viongozi kujiepusha na lugha ya matusi,uchochezi na kashfa katika kampeni zao.

Sauti ya Jaji Francis Mutungi.

Pia amesisitiza vyama vya siasa viwe mabalozi wa kuimarisha amani na mshikamano katika Taifa.

Sauti ya Jaji Francis Mutungi.
Ni muhimu kwa viongozi kujiepusha na lugha ya matusi,uchochezi na kashfa katika kampeni zao.

Ikumbukwe kuwa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa madiwani, wabunge na urais zitafanyika kuanzia Agosti 28 hadi Oktoba 28, siku inayofuata Jumatano, Oktoba 29, 2025 itakuwa siku ya upigaji kura.

Kwa sasa vyama 18 vinavyoshiriki uchaguzi huo, vinaandaa wagombea wa nafasi hizo. Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imekwisha fungua dirisha la uchukuaji na urejeshaji fomu hizo.

Uchukuaji wa fomu za uteuzi wa  urais ulianza Agosti 9 hadi Agosti 27, 2025 huku  ubunge na udiwani limefunguliwa kuanzia Agosti 14 hadi Agosti 27, 2025.