Dodoma FM

Wananchi Malechela waiomba serikali kuwakumbuka nishati safi

18 August 2025, 12:48 pm

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea na jitihada mbalimbali za uelimishaji, uhamasishaji na usambazaji wa bidhaa za Nishati Safi za Kupikia katika Mikoa yote Tanzania Bara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali .Picha na REA.

Fursa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia itawapunguzia wanawake kutumia muda mrefu wa kutafuta kuni kwaajili ya kupikia.

Na Victor Chigwada.
Wananchi wa vitongoji vya Sokoine na Malechela wameiomba Serikali kuwakumbuka katika miradi ya uhamasishaji wa matumizi ya Nishati mbadala kama amabavyo baadhi ya maeneo wananufaika na mpango huo.

wamesema kupitia mpango huo itawapa fursa wananchi wa vijijini kuacha kuharibu mazingira kwa kukata miti kwaajili ya matumizi ya kuni.

Aidha wamesema kuwa fursa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia itawapunguzia wanawake kutumia muda mrefu wa kutafuta kuni kwaajili ya kupikia.

Sauti za wananchi.

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Mnase Ayubu Malima amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto ya uvamizi wa mazingira wameendelea kutoa elimu kwa wananchi

Sauti ya Bw.Ayubu Malima