Dodoma FM

‘Askari wanawake ni tija kwa taifa’

16 July 2025, 3:17 pm

Picha ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Gallus Hyera akiongea wakati akifungua hafla ya mafunzo ya polisi mtandao wanawake. Picha na Lilian Leopord.

Hata hivyo ikumbukwe kuwa askari wa kike ni mama kama mama wengine na wanafanya majukumu yao ya kila siku ya kuhudumia familia na watoto ukiachilia mbali na majukumu yake ya kazi.

Na Lilian Leopord.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Gallus Hyera amesema uwepo wa askari wanawake imekuwa tija kwa taifa kwani wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha amani, ulinzi na usalama unakuwepo.

Kauli hiyo ameitoa jijini Dodoma wakati akifungua hafla ya mafunzo polisi mtandao wanawake yaliyo wakutanisha askari wanawake Mkoa wa Dodoma ambapo amesema jeshi linatamani askari wa kike wawe mstari wa mbele kufanikisha zoezi la ukamati wahalifu wa kike.

Picha ni Kamishana Msaidizi wa Polisi ambaye ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Mkoa wa Dodoma Eva Michael akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa semina hiyo.Picha na Lilian Leopold.
Sauti ya Gallus Hyera

Kamishana Msaidizi wa Polisi ambaye ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Mkoa wa Dodoma Eva Michael ameelezea lengo la semina hiyo ni kuwakutanisha pamoja askari wa kike na kuiondolea jamii dhana potofu iliyo jengeka kwao .

Sauti ya Eva Michael .

Nao washiriki wa semina hiyo wamesema wameelezea jinsi walivyonufaika na mafunzo hayo.  

Sauti ya washiriki.