Dodoma FM

Wananchi waendelee kupatiwa elimu athari ya dawa za kulevya

25 June 2025, 3:46 pm

Picha ni Mkuu wa mkoa wa Dodoma mh Rosemery Senyamule akiwa katika maadhimisho hayo.Picha na Anwary Shaban.

Mwezi juni kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya kupiga vita dawa za kulevya ambapo maadhimisho hayo hufanyika kwa siku tatu mfululizo kuanzia june 24 ,25 na 26

Na Anwary Shaban.

Katika kuadhimisha siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani wananchi mkoani  Dodoma wamehimizwa kupata elimu ya athari za matumizi ya dawa hizo.

Wito huo umetolewa na mkuu wa mkoa wa Dodoma Mh. Rosemary  Senyamule wakati akizungumza na wananchi katika ukumbi wa Jakaya kikwete jijini Dodoma yanapo fanyika maadhimisho hayo.

Mh.Senyamule amesema dawa za kulevya ni janga linalo athiri familia nyingi nchini ,hivyo ni muhimu kwa wananchi kushiri kikatika maonesho hayo.

Sauti ya Mh. Senyamule.
Picha ni Baadhi ya wananchi wakiwa katika maadhimisho hayo.Picha na Anwary Shaban.

Aidha Mh.Senyamule amebainisha lengo la maadhimisho hayo kuwa ni kupaza sauti kwa umma juu ya madhara ya matumizi ya dawa za kulevya.

Sauti ya Mh. Senyamule.

Mwezi juni kila mwaka Dunia huadhimisha siku ya kupiga vita dawa za kulevya ambapo maadhimisho hayo hufanyika kwa siku tatu mfululizo kuanzia june 24 ,25 na 26 ambapo kilele cha maadhimisho hayo kwa hapa nchini kinatarajiwa kufanyika jijini Dodoma huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.