Dodoma FM

Mabadiliko ya tabianchi yanavyo sababisha ukatili wa kijinsia kwa wanawake

18 June 2025, 1:25 pm

Picha ni baadhi ya wanawake wa Kijiji cha Chali Igongo wakiwa katika moja ya kisima kwaajili ya kupata huduma ya maji.Picha na Mariam Kasawa.

Simulizi yetu inatupeleka katika kijiji cha Chali Igongo, wilayani Bahi mkoani Dodoma

Katika maeneo mengi ya vijijini nchini Tanzania, mabadiliko ya tabia nchi yamekuwa tishio la kweli si kwa mazao tu, bali kwa maisha ya kila siku ya wanawake na watoto.

Ukame umegeuka kuwa mgeni wa kudumu. Vyanzo vya maji vinaendelea kukauka. Wanawake wanalazimika kutembea zaidi ya kilomita tano kusaka tone la maji jukumu ambalo kwa miongo mingi limeonekana kuwa la kawaida, lakini sasa limejaa hatari.

Hatari ya kubakwa, kupigwa, au kutukanwa njiani wakati wa kutafuta maji ni changamoto inayowakumba wanawake wengi. Ukatili huu wa kijinsia unaochochewa na mazingira siyo tu kwamba unafichwa, bali pia haujatambuliwa kwa kina katika sera na mikakati ya kitaifa.

Wanawake wa kijiji cha chali Igongo hulazimika kutembea masaa mawili hadi matatu kutafuta maji kila siku.Picha na Mariam Kasawa.

Msikilizaji leo katika Makala yetu tunaangazia suala la mabadiliko. Katika sura ya ukame na uhaba wa maji ambao unachochea kwa kiasi kikubwa katika kuchangia vitendo vya ukatili hasa katika sehemu za vijijini.

Katika makala hii, tutasikia simulizi za wanawake waliokumbwa na madhila hayo, tutazungumza na viongozi wa kijiji, wataalamu wa kijinsia, pamoja na wanaharakati wanaopigania haki za wanawake vijijini.

Ukame umepelekea pia wananchi hawa kutumi maji ambayo si safi na salama kutokana na visima hivi pia kutumiwa na wanyama. Picha na Mariam Kasawa.