Dodoma FM

Serikali yatoa bilioni 51 ukarabati wa miradi ya maendeleo Zanka

5 June 2025, 4:49 pm

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kasper Mmuya akiongea wakati wa maadhimisho hayo. Picha na Anwary Shaban.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Samia Day yaliyofanyika katika Wilaya ya Bahi, Kata yaZanka, Mhe. Kasper amesema fedha hizo zimeboresha miradi mbalimbali ikiwemo ya elimu na afya.

Na Anwary  Shaban .  

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma Bw. Kasper Mmuya amesema katika kipindi cha miaka minne cha Rais Samia Suluhu Hassan jumla ya bilioni 51, 868, 901.17 zilitolewa kwa Wilaya ya Bahi, Kata ya Zanka.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Samia Day yaliyofanyika katika Wilaya ya Bahi, Kata yaZanka, Mhe. Kasper amesema fedha hizo zimeboresha miradi mbalimbali ikiwemo ya elimu na afya.

Sauti ya Mmuya.
Picha ni wakazi wa Zanka wakiwa katika maadhimisho hayo. Picha na Anwary Shabani.

Kwa upande wake, Joyce Paul Manyanda AfisaUtumishi amempongeza Rais Samia Suluhu kwa uboreshaji wa miradi ya elimu, hususani ujenzi wa vyumba vya madarasa.

Sauti ya Joyce Paul Manyanda.

Naye  Mwenyekiti wa kata hiyo Bw. Shaban Hassan na wananchi wamemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uboreshaji wa miradi katika kata hiyo.

Sauti Bw. Shaban Hassan.