Dodoma FM

Ubovu wa barabara ya Ihumwa kubaki historia

6 May 2025, 5:49 pm

Mavunde ameongeza kuwa hapo awali kulikiw na mvutano kati ya TANROAD na TARULA ni nani mwenye kusimamia lakini tayari wamefikia makubaliano.Picha na Google.

Ikumbukwe barabara hiyo ilitangazwa kuweka kiwango cha lami na aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Hayati John pombe Magufuli alipo kuwa akizindua ujenzi wa reli mwendo kasi kutoka Morogoro Hadi Makutupola.

Na Victor Chigwada.

Imeelezwa changamoto ya ubovu wa barabara ya Ihumwa huenda ukabaki stori baada ya Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini Mh.Antony Mavunde kusema kuwa tayari barabara hiyo imeshakabidhiwa TANROAD tayari kuanza kushughulikiwa

Mavunde amesema kuwa mpango huo utatekelezwa haraka iwezekanavyo kutokana na agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dkt.Samia Suluhu Hassan kuwa barabara zote zinazo unga SGR ziwekwe kiwango cha lami

Ameongeza kuwa baada ya barabara hiyo kuwa kwenye mpango Kwa muda mrefu lakini Sasa hatua imefikia pazuri hivyo ni suala la TANROAD kutafuta mkandarasi wa kujenga barabara hiyo Kwa kiwango cha lami

Sauti ya mh. Mavunde.

Aidha Mavunde ameongeza kuwa hapo awali kulikiw na mvutano kati ya TANROAD na TARULA ni nani mwenye kusimamia lakini tayari wamefikia makubaliano na TANROAD ambao wanashughulikia kupatikana Kwa mkandarasi

Sauti ya mh.Mavunde.

Nao baadhi ya wananchi wametoa ombi lao kwa Serikali na TANROAD kuhakikisha ujenzi huo unaanza mara moja kabla ya msimu wa masika kwani ifikapo nyakati hizo mawasiliano Huwa ni magumu

Sauti za wananchi.