Dodoma FM

Mlodaa waomba serikali kuingilia kati ongezeko bei za vyakula

29 April 2025, 6:15 pm

Hali inayo inawaumiza walaji pamoja na wafanyabiashara. Picha na Google.

licha ya kuwa bado tuko mwezi wa nne lakini tayari baadhi ya familia zimeanza kulala na njaa

Na Victor Chigwada.

Wakazi wa Kijiji Cha Mlodaa Kata ya Mlowa barabarani Wilaya ya Chamwino wameiomba Serikali kuingilia kati ili  kupunguza ongezeko la bei za vyakula kwani ni hatari Kwa wananchi wa Hali ya chini.

Bi Fatima Rahim ni mama mpambanaji katika uuzaji wa chakula anaeleza namna ambavyo wanaathilika na kupanda Kwa bei ya mahindi pamoja mchele

Hali inayo inawaumiza walaji pamoja na wafanyabiashara hii yote ni kutokana ukame ulio sababishwa na uhaba wa mvua

Sauti ya Bi. Fatima.

Naye Anna Malindo ameongeza kuwa hali ya kuongeza bei ya bidhaa za chakula inawa gharimu watafutaji wa hali ya chini na kushindwa kuendesha maisha

Sauti ya Anna Malindo.

Mwenyekiti wa kijiji cha Mloda Ndg.Adam Philimini amekiri Moja ya maeneo yaliyo athilika na uhaba wa mvua ni Kijiji chake Cha Mloda hivyo ni vyema Serikali kuwasaidia mahindi ya bei nafuu

Philimini amesema kuwa licha ya kuwa bado tuko mwezi wa nne lakini tayari baadhi ya familia zimeanza kulala na njaa jamboa ambalo ni hatari Kwa miezi ya mbele

Sauti ya Mwenyekiti.