Dodoma FM

Wanafunzi Kidoka waepukana na adha ya kufuata shule umbali mrefu

24 April 2025, 5:31 pm

Picha ni maabara ambayo inapatikana katika shule hiyo mpya ya sekondari inayopatikana Kidoka wilayani Chemba.Picha na Kitana Hamis.

Ujenzi wa shule hiyo umegharimu zaidi ya shilingi milioni 500.

Wanafunzi 320 wa kata ya kidoka wilayani chemba mkoani dodoma, wameondokana na  adha ya kutembea umbali mrefu zaidi ya km 14 kwa sikukufuata shule kata ya jirani .

Hapo awali wanafunzi hao walilazimika kutembea umbali mrefu kuifuata shule maeneo ya kambi ya nyasa hali iliyo hatarisha usalama wao.

Serikali imetatua changamoto hiyo ya shule kwa kujenga shule katika eneo hilo ambayo imegharimu zaidi ya shilingi milioni 500.

Picha ni Mwenge wa uhuru ambapo umezindua shule hiyo pamoja na niradi mbalimbali wilayani Chemba.Picha na Kitana Hamis.
Habari kamili.