Dodoma FM

Miradi ya zaidi ya bilioni 7 yajengwa katika kata ya Miyuji Dodoma

7 April 2025, 5:18 pm

kukamilika kwa miradi hiyo kumepunguza changamoto za kiafya, usafiri na elimu zilizokuwa zikiwakabili wananchi wa kata hiyo. Picha na Alfred Bulahya.

Miradi hiyo ni mradi wa barabara ya lami inayounganisha kata hiyo na Ipagala, zahanati ya Mpamaa, Shule ya Sekondari miyuji, na sule ya msingi mlimwa C.

Na Alfred Bulahya.
Kamati ya siasa kata ya Miyuji ikiongozwa na Diwani wa kata hiyo imefanya ziara ya kutembelea miradi 4 iliyojengwa ndani ya kata hiyo katika kipindi cha miaka 5 ya serikali ya awamu ya sita.

Akiongea baada ya kukamilisha ziara hiyo diwani wa kata hiyo Bi Beautice Ngelangela amesema kukamilika kwa miradi hiyo kumepunguza changamoto za kiafya, usafiri na elimu zilizokuwa zikiwakabili wananchi wa kata hiyo.

Sauti ya Diwani.

Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mpamaa amesema kwa sasa wanahudumia wagonjwa wengi ikilinganishwa na hapo awali huku wakuu wa Shule za Mlima C na Miyuji wakieleza namna itakavyoongeza ufaulu.

Sauti ya Mganga mkuu.
Picha ni diwani wa kata ya Miyuji Bi Beautice Ngelangela akiongea katika ziara hiyo.Picha na Alfred Bulahya.

Wenyeviti wa Mitaa ya Miyuji Propa na Mpamaa wakaeleza furaha yao kutokana na miradi hiyo mikubwa kujengwa ndani ya mitaa yao.

Sauti za wenyeviti

Wananchi nao wanasema kuhusu usafiri, na huduma za Afya hali ni shwari kwa sasa.

Sauti za wananchi.