Dodoma FM

‘Wananchi wapatiwe elimu ya fursa za taka’

1 April 2025, 6:25 pm

elimu ya fursa zitokanazo na taka inapaswa kuwafikia wananchi mbalimbali na kuwanufaisha .Picha NEMC

BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), linawataka Watanzania kuanza kubadili mtazamo na kuziona taka kama fursa ya kuzirejeleza na kupata bidhaa mbalimbali na kujikomboa kiuchumi.

Na Mariam Kasawa.
Mamlaka za serikali za mitaa na halmashauri za wilaya nchini kote zimetakiwa kuhakikisha wananchi wanapata elimu na kutambua kuwa taka ni fursa.

Jamii imekuwa na uelewa mdogo juu ya fursa inayopatikana katika taka ambazo nyingi huishia kurundikwa mahali pamoja au kuzagaa mtaani hivyo kusababisha uchafuzi wa mazingira.

Naibu waziri ofisi ya makamu wa Rais Muungano na mazingira mh. Khamis Hamza Khamis amelitaka baraza la uhifadhi na usimamizi wa mazingira kuhakikisha elimu ya fursa zitokanazo na taka inawafikia wananchi mbalimbali na wananufaika .

Sauti ya mh. Khamis Hamza Khamis.

Aidha amesema taka nyingi zimekuwa zikirundikwa na kusababisha uchafu na harufu mbaya mitaani .

Sauti ya mh. Khamis Hamza Khamis.