Dodoma FM

Fahamu madhara ya vidonge vya P2

9 October 2024, 6:25 pm

Na Lilian Leopord.

Matumizi ya vidonge vya P2 mara kwa mara kama mpango wa dharula wa kuzuia mimba imelelezwa kuwa na madhara makubwa katika suala zima la lafya  ya uzazi.

Akiongea na Dodoma TV, Daktari Fransis Mbwilu kutoka katika kituo cha UMATI  Dodoma amesema kuwa madhara yanayojitokeza endapo mwanamke atajenga mazoea ya kutumia  vidonge vya P2 mara kwa mara  ili kuzuia mimba ni pamoja na kupata hedhi isiyo na mpangilio.

Daktari Fransis Mbwilu kutoka katika kituo cha UMATI  Dodoma
Sauti ya Dkt.  Fransis Mbwilu

Aidha Dkt.  Fransis Mbwilu ameeleza jitihada wanazozichukua ili kutoa elimu kwa jamii juu ya matumizi sahihi ya vidonge vya  P2 ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza endapo mwanamke atajenga mazoea ya matumizi ya vidonge hivyo.

Sauti ya Dkt.  Fransis Mbwilu

Wakitoa maoni yao kwa nyakati tofauti, wananchi wameomba elimu zaidi itolewe ili kujua matumizi sahihi ya vidoge vya P2 ili kuepuka madha yanayoweza kujitokeza.

Pichani mwananchi akieleza juu ya umuhimu wa elimu matumizi sahihi ya P2
Sauti za wananchi
Pichani mwananchi akitoa maoni yake juu ya matumizi ya P2