Dodoma FM

Maelezo na taarifa ya ugonjwa ni wajibu na haki ya mgojwa

19 September 2024, 7:51 pm

Uelewa wa baadhi ya watu kufahamu haki zao za msingi wanapokuwa katika vituo vya afya na hospitali bado ni mdogo. Hali hii ni kutokana na uhaba wa elimu juu ya suala hilo pamoja na baadhi yao kutokuwa na utamaduni wa kuuliza juu ya huduma wanayopatiwa.

Picha ya mwamachi akieleza juu ya uelewa wake kuhusu haki za msingi za mgojwa
Sauti za wananchi
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa  Prof. Abel Makubi 

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa  Prof. Abel Makubi  amewaomba wagonjwa kutoa maelezo sahihi ya ugonjwa na pia na kuwataka  kuomba taarifa toka kwa madaktari mara wanapohudumiwa.

Sauti ya Prof. Abel Makubi 

Mmgonjwa hapaswi kukubali matibabu bila ya kufahamu kikamilifu maelezo ya kina kuhusu athari zinazoweza kutokea, faida za matibabu na mbadala wa matibabu yanayopendekezwa na pia kuwepo na siri baina ya mgonjwa na daktari

Jamii inashauriwa kutopuuza maumivu au dalili mbaya watakazohisi katika miili yao kwani kunasababisha kuchelewa kupata matibabu ili hali ugonjwa ukizidi kukua na kusababisha athari kwa mgojwa.

Kila septemba 17 ya kila mwaka ni maadhimisho ya siku ya usalama wa mgonjwa duniani, lengo ikiwa ni kuzingatia usalama wa mgonjwa kwa kuanzisha na kuimarisha mifumo inayotegemea sayansi, kuboresha usalama wa wagonjwa na ubora wa huduma za afya.

Picha kuonesha wanachi wakiwa katika mchakato wa matibabu