Dodoma FM

Polisi Dodoma kushirikiana na wauzaji, mafundi simu kuzuia uhalifu

14 April 2025, 5:36 pm

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, George Katabazi akiongea na wandishi wa habari baada ya semina hiyo.Picha na Lilian Leopord.

Aidha Kamanda wa Jeshi la Polisi amewataka wananchi kuacha tabia ya kupokea mali za wizi na iwapo watangundua tukio lolote la uhalifu watoe taarifa katika mamlaka husika.

Na Lilian Leopord.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, George Katabazi amesema kuwa matukio ya wizi wa mali ikiwemo simu umeendelea kukua katika Jiji la Dodoma.

Katabazi ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati alipokutana na wauzaji na mafundi wa simu na tv zilizotumika lengo ikiwa ni kubaini na kutatua changamoto za uhalifu.

Sauti ya kamanda Katabazi.

Aidha Katabazi amebainisha maazimio waliyoyaweka katika kukabiliana na uhalifu ikiwemo kuendeleza ushirikiano na kufanya kazi kwa kuzingatia nidhamu, haki, weledi na uadilifu.

Sauti ya kamanda Katabazi.

Kwa upande wake Meneja wa Kitengo cha Masuala ya Wateja na Watumiaji ya Mamlaka ya Hali ya Mawasiliano Tanzania ( TCRA) Kadaya Balugye, amesema kutokana na takwimu zilizokuwa zikitolewa na TCRA kuanzia mwezi Juni majaribio ya ulaghai wa mtandao katika Mkoa wa Dodoma unaendelea kupungua.

Picha ni Meneja wa Kitengo cha Masuala ya Wateja na Watumiaji wa Mamlaka ya Hali ya Mawasiliano Tanzania ( TCRA) Kadaya Balugye.Picha na Lilian Leopord.
Sauti ya Kadaya Balugye,

Baadhi ya wauza simu na mafundi simu waliojitokeza katika kikao hicho wamesema kuwa kutokana elimu waliyoipata itawasaidia sana na kupunguza idadi ya uhalifu.

Sauti za mafundi.