Dodoma FM

Betri chakavu za magari ni hatari kwa afya

23 October 2024, 12:55 am

Na Mariam Kasawa.

Taka za betri chakavu zinatajwa kuwa na athari kimazingira na kiafya kwa binadamu hivyo  umakini unahitajila katika kuziteketeza au kurejelezwa.

Akizingumza katika wiki ya kujiondosha  na kuepukana na taka za As lead zinazotokana na betri chakavu, Bwn . Hamad Taimuru Meneja Uzingatiaji Baraza la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC  amesema viwanda vyote vinatakiwa kufanya  tathini ya athari kwa mazingira ili kujua miiko iliyowekwa ya urejelezaji wa taka.

Bwn . Hamad Taimuru Meneja Uzingatiaji Baraza la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC
Sauti ya Bwn . Hamad Taimuru

Aidha amesema  wamekutana na wadau mbalimbali wakiwemo wamiliki wa viwanda ili waweze kuona urejezeji wa betri chakavu unavyo fanyika katika viwanda.

Pichani wadau wenye viwanda wakishiriki wa warsha ya mazingira
Sauti ya Bwn . Hamad Taimuru

Taka za betri chakavu zinatajwa kuwa na athari kimazingira na kiafya kwa binadamu hivyo zinapaswa kuteketezwa au kurejelezwa ili zisilete athari katika mazingira.