Dodoma FM

Mrundikano wa taka soko la samaki Bonanza wahatarisha afya za wananchi

20 December 2023, 4:43 pm

Picha ni mazingira ya soko hilo hususani msimu huu wa mvua za masika. Picha na Thadei Tesha.

kwa mujibu wa wafanyabiashara wa soko hili wanadai ni muda mrefu tangu kuanza ujenzi wa soko hili na iwapo litakamilika linatarajiwa kupunguza athari mbalimbali wanazopitia wafanyabiashara hao.

Na Thadei Tesha
Wafanyabiashara wa soko la Bonanza Jijini Dodoma wameulalamikia uongozi wa Jiji la Dodoma kwa kuchelewa kukamilika kwa mradi wa soko jambo linaloweza kusababisha athari za magonjwa ya mlipuko hususani kipindi hivi cha mvua.

Dodoma tv imefika katika soko hili nakushuhudia mbali na shuguhli za kuuza samaki zikiendelea, mazingira ya soko hili bado si rafiki hivyo kuwalazimu wafanyabiashara hawa kuuza bidhaa zao wakiwa wamepang chini licha ya wadudu kuonekana wakizagaa maeneo hayo.

Sauti yawananchi soko la bonanaza.
Picha ni wafanyabishara na wanunuzi wa samaki katika soko hilo. Picha na Thadei Tesha.

Inaelezwa kuwa ni muda mrefu tangu ujenzi wa soko jipya la samaki ufanyike katika eneo hili lakini hadi sasa bado halijakamilika je, uongozi wa soko hili wamechukua hatua gani?

Sauti ya ofisi ya soko la bonanaza

Inanilazimu kufunga safari hadi katika ofisi ya mkurugenzi wa jiji la dodoma kwa ajili ya kutolea ufafanuzi wa kina juu ya suala hili.

Bw abeid Msangi ni kaimu mkuu wa divisheni ya viwanda na biashara katika jiji la Dododma hapa anaeleza mikakati ya jiji kuboresha miundombinu ya soko hilo.

Sauti ya Bw abeid Msangi .