Dodoma FM

Ujenzi wa shule Matumbulu watatua kero ya wanafunzi kutembe umbali mrefu

30 April 2025, 6:03 pm

Mlezi wa Shule Mwalimu Zedekia Agutu akisoma taarifa ya mradi huo.Picha na Lilian Leopord.

Mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 544 laki mbili ishirini na tano mia sita ishirini na sita (544, 225, 600) kwa  ajili ya ujenzi wa miundombinu.

Na lilian Leopord.

Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Matumbulu umetajwa kutatua changamoto ya wanafunzi waliokuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma ya elimu.

Akisoma taarifa ya mradi, Mlezi wa Shule Mwalimu Zedekia Agutu amesema mradi huo utakamilika mwezi Mei 2025, na mpaka sasa baadhi ya wanafunzi wameshaanza masomo.

Sauti ya Mwalimu Zedekia Agutu.
Picha ni Moja ya Jengo la shule hiyo ambalo limejengwa kupitia mradi huo.Picha na Lilian Leopord.

Naye Diwani wa Kata ya Matumbulu, Emmanuel Chibago ameiomba halmashauri kurekebisha barabara ili wanafunzi waweze  kufika shuleni kiurahisi.

Sauti ya Mh Emmanuel Chibago.

Kwa upande wake Daud Mkhandi Kiongozi wa Kamati ya Fedha na Utawala amebainisha mipango yaliyoiweka katika kuhakikisha shule hiyo inakua na usalama.

Sauti ya Daudi Mkhandi