Dodoma FM

Wizara ya Afya yapunguza 70% rufaa za matibabu nje ya nchi

21 October 2024, 7:35 pm

Na Mariam Kasawa

Mpango wa serikali  wa miaka mitano 2020-2025  kusomesha wataalam bingwa na wabobezi  300 kila mwaka, umepunguza kwa 70% rufaa za matibabu nje ya nchi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Waziri wa Afya Mh. Jenista Mhagama  anabainisha mipango ambayo wizara imejiwekea  ili kuimarisha afya sekta ya afya.

Pichani Waziri wa Afya Mh. Jenista Mhagama akielezea mikakati ya wizara ya afya
Sauti ya Mhe. Jenista Mhagama

Aidha Mh. Mhagama amesema jitahada hizi zinazo fanywa katika sekta ya afya zinalenga kupunguza rufaa za matibabu nje ya nchi na kupunguza gharama za matibabu.

Pichani waandishi wa habari katika kikao cha waziri wa afya Mhe. Jenista Muhagama
Sauti ya Mhe. Jenista Mhagama
Pichani baadahi ya washiriki wa kikao cha wizara ya afya

Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali Watu, Wizara ya Afya Dkt. Saitori Laizer, akajibu baadhi ya maswali yaliyo ulizwa na waandishi wa habari kuhusu rufaa za nje.

Pichani Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali Watu, Wizara ya Afya Dkt. Saitori Laizer
Sauti ya Dkt. Saitori Laizer

Serikali imejiwekea lengo la miaka mitano 2020-2025 la kusomesha wataalamu bingwa na wabobezi wasio pungua 300 kwa kila mwaka wa fedha kupitia ufadhili wa masomo wa serikali unaojulikana kama Samia Health Specialization Scholarship Program.