Storm FM

GGML yafadhili pedi 5,000 kwa wanafunzi kutoka shule 56 mkoani Geita

30 May 2026, 6:15 pm

Mkurugenzi wa GGML Ashraf  Suryaningrat akizungumza na washiriki (hawapo pichani) maadhimisho siku ya hedhi salama. Picha na Ester Mabula

GGML imeendeleza dhamira yake ya kuikumbuka na kurejesha kwa Jamii kwa kugusa makundi mbalimbali kupitia ufadhili wa elimu pamoja na vifaa kwa wanafunzi wa kike mkoani Geita.

Na: Ester Mabula

Kampuni ya GGML (Geita Gold Minning Limited) imefadhili jumla ya Pedi 5000 zenye thamani ya shilingi miliion 42 kwa wanafunzi wa kike kutoka katika shule za msingi na sekondari 56 zilizopo mkoani Geita.

Zoezi la ugawaji wa pedi hizo limeendana na utoaji wa elimu kuhusu hedhi salama kwa wanafunzi hao ambalo limefanyika Mei 28, 2026 kwenye ukumbi wa St. Aloysius manispaa ya Geita ikiwa ni maadhimisho ya siku ya hedhi salama.

Mgeni rasmi akiongoza zoezi la ugawaji wa taulo za kike kwa wanafunzi baada ya kupewa elimu ya hedhi salama. Picha na Ester Mabula

Akizungumza wakati wa programu hiyo, mwakilishi wa GGML Elibariki Jambau pamoja na mkurugenzi wa GGML Ashraf  Suryaningrat  wamesema lengo la elimu hiyo ni kuwajengea wanafunzi uelewa sahihi kuhusu hedhi, kuondoa unyanyapaa pamoja na kupunguza utoro kwa wanafunzi wa kike.

Sauti ya wwakilishi pamoja na mkurugenzi wa GGML

Mgeni rasmi, Kamanda wa polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo ametoa pongezi kwa GGML kwa kuendelea kuimkumbuka Jamii na kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuwezesha mazingira bora kwa wanafunzi wote.

Sauti ya mgeni rasmi, SACP Safia Jongo
Mgeni rasmi, Kamanda wa polisi mkoa wa Geita SACP Safia Jongo akitoa hotuba yake kwa washiriki. Picha na Ester Mabula

Baadhi ya wanafunzi waliopewa elimu hiyo wameeleza kunufaika na kwamba watatumia elimu hiyo kuwaelimisha wazazi na Jamii kuachana na imani potofu juu ya hedhi.

Sauti ya wanafunzi
Angel Lucas, mwanafunzi wa shule ya sekondari Nyanza akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Programu hiyo ni sehemu ya shughuli za kijamii zinazotekelezwa na GGML kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu na afya katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mazingira bora ya kujifunza.