Storm FM
Storm FM
20 June 2026, 6:55 pm

Kituo hicho kitakuwa kikiendesha shughuli zake katika viwanja vya shule ya sekondari ya Waja boys iliyopo halmashauri ya manispaa ya Geita chini ya kocha Choki Abeid pamoja na makocha wengine wenye uzoefu wa kuibua vipaji vya watoto.
Na: Ester Mabula
Kituo cha Twist Elite Football Academy kimefunguliwa rasmi leo Juni 20, 2026 kwaajili ya kutoa mafunzo ya mpira wa miguu kwa watoto wadogo kuanzia umiri wa miaka minne hadi 15.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kituo hicho Mkurugenzi wa Twist Elite Football Academy Ndg. Ally Twist ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Geita (GEDFA) amesema dhamira ya kituo hicho ni kuendeleza vipaji vya watoto na kuwalea katika misingi bora.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika uzinduzi huo Bi. Juliana Kimaro, Afisa michezo halmashauri ya manispaa ya Geita amempongeza mkurugenzi kwa kuanzisha kituo hicho huku akitowa wito kwa wazazi kuchangamkia furasa hiyo ili kuwatengenezea watoto wao msingi mzuri wa maisha ya bàadae.
Baadhi ya wazazi na walezi waliopeleka watoto wao katika kituo hicho wamepongeza hatua hiyo na kueleza itawasidia katika kuibua na kuendeleza vipaji vya watoto wao.
