Storm FM
Storm FM
12 December 2025, 12:12

Vipaumbele vikubwa vya fedha hizo za CSR ni huduma za Afya kwakuwa kata hizo zina ongezeko kubwa la watu kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini.
Na Mrisho Sadick:
Wakazi wa Kata nne za Halmashauri ya wilaya ya Geita Mkoani Geita wanatarajia kunufaika na fedha za CSR zaidi ya milioni 600 kutoka mgodi wa dhahabu wa Bucreef unaofanya shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu katika eneo hilo.
Wakizungumzia hatua hiyo baadhi ya wananchi kutoka Kata za Lwamgasa , Kaseme , Busanda na Butundwe wanaotarajia kunufaika na fedha hizo katika hafla ya utiaji saini wa makubaliano ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kutokana na fedha hizo na mgodi wa Bucreef , zoezi ambalo limeshuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela wamesema fedha hizo zitakuwa chachu ya maendeleo.

Meneja Mkuu wa Mgodi wa Bucreef Isack Bisansaba amesema vipaumbele vikubwa vya fedha hizo za CSR ni huduma za Afya kwakuwa kata hizo zina ongezeko kubwa la watu kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu huku mkuu wa wilaya ya Geita Hashim Komba akiahidi kuendelea kuwalinda wawekezaji kwakuwa wamekuwa chachu ya maendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Martine Shigela ameupongeza Mgodi huo kwa kuendelea kutekeleza miradi ya huduma za Jamii bila changamoto huku akiwataka watendaji wa serikali na Wananchi kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha fedha hizo zinawanufaisha.