Storm FM

Eng. Chacha, Sukambi waahidi kuijenga Nyankumbu mpya

10 October 2025, 05:37

Mgombea udiwani Paschal Sukambi (kushoto) na mgombea ubunge Chacha Wambura (kulia). Picha na Ester Mabula

“Chacha ni Nzagamba lililoshiba, liko tayari kwaajili ya kuleta maendeleo katika jimbo la Geita mjini na kuendeleza kutekeleza ilani ya CCM” – Chacha Wambura

Na: Ester Mabula

Katika mwendelezo wa kampeni za mgombea ubunge jimbo la Geita mjini kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Mhandisi Chacha Mwita Wambura, Oktoba 09, 2025 ilikuwa zamu ya kata ya Nyankumbu.

Wananchi wa kata ya Nyankumbu waliojitokeza katika mkutano wa kampeni. Picha na Ester Mabula

Akizungumza na wakazi wa kata hiyo na wananchi waliojitokeza kumsikiliza, ameeleza kuwa dhamira yake kuu ni kuleta maendeleo katika jimbo la Geita sambamba na kutatua changamoto ya miundombinu ambayo imekuwa kikwazo katika kata hiyo.

Sauti ya mhandisi Chacha Wambura
Mgombea ubunge jimbo la Geita mjini (CCM) Mhandisi Chacha Mwita Wambura akizungumza na wananchi wa Nyankumbu (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula

Naye mgombea udiwani wa kata hiyo kwa tiketi ya CCM Paschal Sukambi ameeleza kuwa iwapo wananchi watamchagua atahakikisha anapambana kupunguza ajali katika barabara kuu ya kata hiyo ambayo imekuwa kikwazo na chanzo kikuu cha ajali.

Sauti ya Paschal Sukambi
Mgombea udiwani kata ya Nyankumbu (CCM) Paschal Sukambi akizungumza na wananchi wa Nyankumbu. Picha na Ester Mabula

Mgeni rasmi katika mkutano huo Nicholaus Kasendamila ambaye ni mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita amesema chama cha mapinduzi kimeendelea kujinasibu kwa kuleta maendeleo na kuwasihi wananchi kuchagua viongozi wa CCM.

Sauti ya mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Nicholaus Kasendamila akizungumza na wananchi wa nyankumbu (hawapo pichani). Picha na Ester Mabula
Wananchi wa kata ya Nyankumbu waliojitokeza katika mkutano wa kampeni. Picha na Ester Mabula