Storm FM
Storm FM
23 May 2026, 4:35 pm

Tamasha la utamaduni na nyamachoma litakuwa likifanyika kila mwezi ili kuenzi mila na desturi sambamba na kutoa fursa kwa wajasiriamali kujiongezea kipato.
Na: Ester Mabula
Uongozi wa halmashauri ya manispaa ya Geita kwa kushirikiana nakampuni ya Geita Gold Minning Limited (GGML) umeandaaa tmasha la utamaduni na nyamachoma ambalo limewakutanisha wakazi wa Geita na maeneo ya kanda ya ziwa kujifunza mila na desturi mbalimbali kupita ngoma za asili, vyakula vya asili na mitindo ya maisha.
Akizungumza Mei 22, 2026 wakati wa ufunguzi wa tamasha hilo Mkurugenzi wa manispaa ya Geita Yefred Myenzi amesema lengo la tamasha hilo ni kuenzi na kuendeleza mila na desturi sambamba na kutoa fursa kwa wajasiriamali.

Makamu wa Rais wa AngloGold Ashanti anayesimamia shughuli za uendelevu na mahusiano ya Kampuni barani Afrika Ndg. Simon Shayo amesema kampuni hiyo inaenzi umoja na ushirikiano kutokana na kufanya kazi na watu wa mataifa mbalimbali.

Akizungumza mgeni Rasmi Mkuu wa mkoa wa Geita Martine Shigela ameipongeza kampuni ya GGML pamoja na viongozi wa manispaa ya Geita kwa kufanikisha tamasha hilo akieleza kuwa tamasha hilo ni mwendelezo wa kuutangaza mkoa wa Geita.
