Storm FM
Storm FM
4 May 2026, 4:59 pm

“Mafanikio ya awamu ya kwanza yalifikia zaidi ya asilimia 100 na tunatarajia hata kwa awamu hii ya pili zoezi letu litakwenda kikamilifu ili watoto waweze kupata chanjo” – Mratibu wa elimu ya Afya kwa UMMA Geita Bi. Paskazia Madulu
Na: Ester Mabula
Serikali kupitia wizara ya Afya inatarajia kuanza kutoa chanjo ya Polio kwa awamu ta pili kwa watoto chini ya umri wa miaka 10 mkoani Geita tangu kukamilika kwa awamu ya kwanza ya utoaji wa chanjo hiyo Marchi 27, mwaka huu.
Maandalizi ya mpango huo yameambatana na utoaji wa elimu kwa watu maarufu kwenye Jamii iliyotolewa leo Mei 04, 2026 ambao wameelishwa juu ya umuhimu wa chanjo hiyo, akizungumza muelimishaji Penford Joel kutoka wizara ya Afya idara ya kinga sehemu ya Afya kwa UMMA amesema awamu hii ya pili itatolewa kwa watoto wote hata ambao waliopata chanjo awamu iliyopita.

Mratibu wa elimu ya Afya kwa UMMA mkoa wa Geita Bi. Paskazia Madulu amesema awamu ya kwanza zoezi hilo lilifanyika kikamilifu na hivyo wana matarajio makubwa kwa awamu ya pili ambayo itaanza Mei 7 hadi 10 mwaka huu huku Mratibu wa Redcross mkoa wa Geita Peter Enock akiwahimiza wazazi na walezi kuwapeleka watoto kupata chanjo hiyo
Baadhi ya washiriki waliopewa elimu hiyo wameeleza kuwa watasaidia kuielimisha Jamii juu ya umuhimu wa chanjo huku wakiipongeza serikali kwa kuendelea kutoa elimu ya kupambana na maradhi mbalimbali.
