Storm FM
Storm FM
28 April 2026, 7:41 am

Serikali ya mtaa wa Mkoani imemkamata mwanamke aliyedaiwa kujisaidia katika diaba lililokuwa na pombe ya kienyeji kwa kile kilichoelezwa ni wivu wa kimapenzi katika eneo la Lukilini mtaa wa Mkoani kata ya kalangalala manispaa ya Geita.
Na: Kale Chongela
Ikumbukwe kuwa tuko hilo lilitokea April 02, 2026 katika mtaa huo ambapo baada ya mwanamke huyo kutendo tukio hilo alitokemea kusikijulikana na baada ya kurejea amejikuta anatiwa nguvuni.
Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo Bw Salvatory Daniel akizungumza na Storm FM amethibitisha kukamatwa kwa mwanamke huyo ambaye jina lake limehifadhiwa na kwamba amefikishwa kituo cha polisi kwa hatua zaidi za kisheria.
Mmiliki wa klabu ya pombe za kienyeji Bi. Elizabeth Francisco amesema kiu yake ni kulipwa gharama za uharibifu uliofanyika kiasi cha shilingi laki 5.
Hata hivyo mwanamke huyo ambaye ametuhumiwa kutenda kosa hilo amekana kutohusika na tukio hilo.
