Storm FM

Mahafali ya 4 ya kidato cha 6 shule ya Shantamine yafana

17 April 2026, 1:56 am

Wahitimu wa kidato cha sita katika shule ya sekondari Shantamine wakiburudika katika sherehe ya mahafali. Picha na Ester Mabula

“Kila Jambo hapa duniani kwa sasa linategemea elimu, hata mimi leo nisingekuwa diwani kama nisingeweka bidii kwenye masomo ili kutimiza ndoto zangu” – Mgeni rasmi Reuben Sagayika

Na: Ester Mabula

Mahafali ya nne ya kidato cha sita yamefanyika Aprili 16, 2026 katika shule ya sekondari Shantamine iliyopo kata ya Mtakuja, manispaa ya Geita ambapo wahitimu wamehimizwa kujiandaa vyema ili kufanya vizuri kwenye mtihani wa kuhitimu.

Awali wakisoma Risala mbele ya mgeni rasmi, Mkuu wa shule msaidizi Mwalimu Petro Nchalangi na Muhitimu wa kidato cha sita Slama Njau wamesema shule hiyo imepiga hatua kitaaluma katika maandalizi ya mitihani ya ndani na nje huku wakieleza changamoto za kitaaluma na kimiundombinu zinazoikabili shule hiyo.

Sauti ya mwalimu na mwanafunzi wakisoma risala
Mkuu wa shule msaidizi Mwalimu Petro Nchalangi akisoma risala mbele ya mgeni rasmi. Picha na Ester Mabula

Mgeni rasmi, Diwani wa kata ya Kalangalala Reuben Sagayika kwa niaba ya mstahiki Meya Leonard Bugomola, ameeleza mikakati ambayo itafanyika ili kutatua changamoto hizo.

Sauti ya mgeni rasmi, Diwani Reuben Sagayika
Mgeni rasmi, Diwani wa kata ya Kalangalala Reuben Sagayika akizungumza katika sherehe ya mahafali. Picha na Ester Mabula

Akizungumza Diwani wa kata ya Mtakuja Costantine Morandi amewapongeza walimu kwa kuendelea kuwajenga wanafunzi kimaadili na kitaaluma jambo linalochochea ufaulu mzuri.

Sauti ya Diwani wa kata ya Mtakuja Costantine Morandi
Mwanafunzi bora kwa ujumla akikabidhiwa cheti cha pongezi na mgeni rasmi. Picha na Ester Mabula