Storm FM
Storm FM
28 April 2026, 7:07 pm

Jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Geita limetoa elimu kwa wanafunzi wa shule za msingi kuelekea siku ya wazima moto Duniani ambayo huadhimishwa kila Mei 04 ya kila mwaka kwa lengo la kuwakumbuka mashujaa waliopotea maisha katika shughuli za uokoaji.
Na: Ester Mabula
Elimu ya kukabiliana na majanga ya moto imetolewa kwa wanafunzi wa shule za msingi Mseto na Bombambili zilizopo katika halmashauri ya manispaa ya Geita.
Akizungumza Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na uokoaji mkoa wa Geita Mrakibu msaidizi Keneth Mwakasitu amesema lengo la kutoa mafunzo kwa wanafunzi wa shule ya msingi ni kuhakikisha elimu inawafikia Jamii kuanzia umri wa utotoni

Walimu wa shule hizo Mwl. Japhet Msilanga na Mwl. Mwanaisha Hamza wametoa pongezi kwa Jeshi la zimamoto na uokoaji kwa kutoa elimu kwa wanafunzi wakieleza itasaidia kuwajengea uelewa zaidi hata katika masomo yao.

Baadhi ya wanafunzi waliopatiwa elimu wamesema watatumia elimu hiyo kuwaelimisha wengine sambamba na kuwakumbusha wazazi kupiga namba ya msaada pindi majanga yanapojitokeza.
Jeshi la zimamoto na uokoaji nchini limeendelea kufikisha elimu kwenye Jamii kwa kuyafikia makundi mbalimbali ambapo Balozi wa zimamoto Mwalimu Yusuph Ibrahim amesema Jamii imeendelea kupata uelewa zaidi tofauti na ilivyokuwa awali.
