Storm FM

Wizara ya Maendeleo ya Jamii kuwainua wafanyabiashara

14 May 2025, 9:31 am

Afisa maendeleo ya Jamii kutoka wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, wanawake na makundi maalumu Carlos Gwamagobe

‘Mikopo hii ina riba nafuu kabisa na ni maono ya serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwainua wafanyabishara kufikia malengo yao’ – Afisa maendeleo ya Jamii Carlos Gwamgobe

Na: Ester Mabula:

Serikali kupitia wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, wanawake na makundi maalumu inatoa mikopo yenye riba nafuu kwa wananchi ili kuwasaidia kuendeleza biashara zao

Akizungumza na waandishi wa habari jana Mei 13, 2025  katika ofisi ya Katibu tawala mkoa wa Geita, Afisa maendeleo ya jamii kutoka wizara hiyo Carlos Gwamagobe amesema watakuwa mkoani Geita kwa siku tatu kwa lengo kuu la kuhamasisha wafanyabishara kuweza kujisajili  kupata vitambulisho ili kupata mikopo hiyo kwani serikali imetenga zaidi ya shilingi bilioni 8 ya mikopo hiyo.

Sauti ya Afisa maendeleo ya Jamii Carlos Gwamgobe
Mwenyekiti wa wafanyabisahara wadogo wadogo maarufu Machinga mkoa wa Geita Maulid Said.

Mwenyekiti wa wafanyabisahara wadogo wadogo maarufu Machinga mkoa wa Geita Maulid Said amesema wafanyabiashara wamehamasika kujisajili ili kupata mikopo lakini changamoto imekuwa ni ucheleweshwaji wa kupewa mikopo hiyo na kushauri changamoto hizo zitatuliwe ili kuweza kurahisisha mchakato huo

Sauti ya mwenyekiti wa wafanyabiashara Maulid Said

Katibu Tawala mkoa wa Geita Mhe. Mohamed Gombati amesema Serikali ya awamu ya sita imeendelea kujipambanua na kuweka mazingira wezeshi kwa wafanyabishara wote na kwamba mikopo hiyo itasiaidia katika kuongeza uchumi wa wafanyabiashara na mkoa kwa ujumla.

Sauti ya Katibu tawala mkoa wa Geita Mohamed Gombati
Katibu tawala mkoa wa Geita Mohamed Gombati akizungumza na waandishi wa habari na maafisa wa mpango huo.