Storm FM
Storm FM
6 June 2025, 17:50

Matamanio ya muda mrefu kwa wakazi wa Manispaa ya Geita yakuahidiwa kituo cha kisasa cha mabasi ya abiria huenda yakafanikiwa baada ya Manispaa hiyo kusaini mkataba wa ujenzi.
Na Kale Chongela:
Halmashauri ya Manispaa ya Geita imesaini mkataba wa ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi ya abiria na kampuni ya SIHOTECH Engineering leo Juni 06,2025 EPZA mjini Geita huku ujenzi huo ukitarajiwa kuanza tarehe 15 ya mwezi huu.
Mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Geita Yefred Myenzi akiwa katika hafla hiyo amesema ujenzi huo utagharimu zaidi ya Bilioni 19 ili kuondoa adha waliyokuwa wakiipata wananchi katika kituo cha sasa hususani kipindi cha mvua.
Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini Costantine Kanyasu amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia kwa kutoa fedha hizo huku mstahiki meya wa Manispaa hiyo Costantine Morandi amewashukuru wananchi kwa kuendelea kuwa wavulivu kwa kipindi kwa kipindi kirefu.

Mkuu wa wilaya ya Geita Hashim Komba kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Geita amepongeza hatua hiyo huku akimtaka mkandarasi anaetekeleza mradi huo kuhakikisha anazingatia muda wa mkataba kwakuwa kituo kinachotumika kwasasa hakikidhi matarajio.