Storm FM

DC Geita aipongeza Storm FM kuhamasisha kampeni ya usafi

10 May 2025, 1:29 pm

Mkuu wa wilaya ya Geita akiwa na kundi la bodaboda katika mwendelezo wa kufanya usafi. Picha na Kale Chongela

Wilaya ya Geita imeendelea na kampeni ya usafi wa mazingira yenye lengo la kuweka manispaa kuwa safi sambamba na kuepuka magonjwa yatokanayo na uchafu.

Na: Kale Chongela:

Mkuu wa wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba ameipongeza redio ya Storm FM kwa kuendelea k,uhamasisha Jamii umuhimu wa kufanya usafi katika maeneo yao ya biashara sambamba na makazi yao kupitia kampeni ya ‘HYAGULAGA GEITA’

Mhe. Komba amesema hayo leo Mei 10, 2025 akiwa katika mtaa wa Nyantorotoro B kata ya Nyankumbu, halmashauri ya Manispaa ya Geita baada ya zoezi la usafi lililokutanisha madereva pikipiki na kundi la wanawake na Samia mkoa wa Geita ambapo amesema Storm FM imekuwa redio bora katika kuhabarisha jamii suala la kufanya usafi wa mazingira.

Sauti ya mkuu wa wilaya ya Geita Hashim Komba
Mkuu wa wilaya ya Geita akizungumza na wananchi waliojitokeza kufanya usafi. Picha na Kale Chongela

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Nyantorotoro B Bw. Juma Seif Ally ametumia fursa hiyo kuwasihi wananchi wa mtaa huo kuhakikisha kila mmoja anafanya usafi katika eneo lake.  

Sauti ya mwenyekiti Bw. Juma Seif Ally

Katibu wa madereva pikipiki kata ya Nyankumbu Bw. Moses Baraka amesema wamelazimika kufanya usafi katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuunga mkono jitihada za mkuu wa wilaya katika kampeni yake ya HYAGULAGA GEITA ikimaanisha SAFISHA/FAGIA Geita .

Sauti ya katibu wa madereva Mosses Baraka

Afisa mazingira Manispa ya Geita Bw. Edward Mwita amesema suala la usafi ni lazima kwa kila mmoja ili kundokana na magonjwa yatokanayo na uchafu.

Sauti ya afisa mazingira Edward Mwita
Mkuu wa wilaya ya Geita akishiriki kuweka taka katika gari la uchafu. Picha na Kale Chongela