Storm FM

Njema Labs wapongeza uwepo wa maonesho ya madini Geita

10 October 2024, 11:10 am

Mkurugenzi wa kampuni ya Njema labs Emmanuel Solomon akiendelea kupokea wananchi mbalimbali wanaofika katika banda lao. Picha na Ester Mabula

Leo ni siku ya 9 tangu kuanza kwa maonesho ya 7 ya teknolojia ya madini mkoani Geita ambayo yameendelea kufanyika kila mwaka yakiwakutanisha watu mbalimbali.

Na: Ester mabula – Geita

Kampuni ya Njema Labs inayojihusisha na upimaji wa sampuli za madini amepongeza uwepo wa maonesho ya madini yanayoendelea katika viwanja vya EPZA Bombambili mjini Geita kwani yanarahisisha watu kupata huduma mbalimbali kwa urahisi na haraka.

Vifaa mbalimbali vinavyotumika katika upimaji wa sampuli za madini. Picha na Ester Mabula

Akizungumza na Storm FM Oktoba 9, 2024 akiwa katika maonesho hayo ameeleza kazi na shughuli mbalimbali wanazofanya kupitia Njema Labs.

Sauti ya meneja

Aidha amesema kuwa maonesho ya mwaka huu yamekuwa na mwitikio mkubwa kuliko ya miaka iliyopita na hivyo yanawasaidia zaidi katika kuendelea kuwafikia watu mbalimbali.

Sauti ya meneja
Mwananchi aliyejitokeza kwaajili ya kupata elimu katika banda la Njema Labs. Picha na Ester Mabula