Storm FM

CCM Geita yapiga marufuku siasa za makundi

6 June 2026, 9:23 pm

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Nikolaus Kasendamila akizungumza na wanachama wa CCM Chato. Picha na Mrisho Sadick

Ujenzi wa ofisi hiyo ni sehemu ya jitihada za kuimarisha shughuli za CCM ngazi ya kata na kuweka mazingira bora ya utekelezaji wa majukumu ya chama

Na Mrisho Sadick:

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Nikolaus Kasendamila amewataka wanachama wa chama hicho kuachana na tofauti zilizojitokeza wakati wa uchaguzi na kuelekeza nguvu zao katika kukijenga chama pamoja na kuimarisha mshikamano miongoni mwa wanachama.

Akizungumza katika Kijiji cha Ichwankima wilayani Chato wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisi ya CCM ya Kata hiyo katika ziara yake ya Kata kwa Kata Kasendamila amesema uchaguzi umekwisha na waliokuwa wakigombea nafasi mbalimbali sasa wanapaswa kufanya kazi kwa pamoja kwa maslahi ya chama.

Sauti ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita
Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa Reuben Sagayika akizungumza na wana CCM Chato. Picha na Mrisho Sadick

Katika hatua nyingine Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa Reuben Sagayika amechangia shilingi milioni moja kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa ofisi hiyo huku akitoa wito kwa wanachama na wananchi kuendelea kushiriki katika maendeleo ya chama na jamii inayowazunguka.

Sauti ya Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM Taifa
Wanachama wa CCM Ichwankima wakiwa kwenye mkutano wa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita kijiji humo. Picha na Mrisho Sadick