Storm FM

Mabasi yagongana na kuua mtu mmoja Nyamigota, Geita

20 June 2026, 5:31 pm

Picha ya baada ya mabasi hayo kugongana katika ajali iliyopelekea kifo cha mtu mmoja. Picha na mwandishi wetu

Jumla ya watu 9 wamejeruhiwa na wengine kunusurika huku mtu mmoja akifariki dunia kutoka na ajali hiyo ambayo ilitokea katika kata ya Nyamigota iliyopo wilaya ya Geita.

Na: Ester Mabula

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 9 kujeruhiwa katika ajali ya mabasi mawili kugongana katika kata ya Nyamigota, mamlaka ya mji mdogo Katoro mkoani Geita.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kenneth Mwakasitu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo mnamo June 19, 2026 akisema ajali hiyo inatajwa kusababishwa na mwendokasi na uzembe wa madereva barabarani.

Mwakasitu ameyataja mabasi yaliyopata ajali kuwa ni ya Kampuni ya Najimnisa iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Geita na Basi la Manyama iliyokuwa ikitokea Jijini Mwanza kuelekea Ngara.

Kaimu kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji mkoa wa Geita
Kaimu kamanda wa Jeshi la Zimamoti na Uokoaji mkoa wa Geita Keneth Mwakasitu akizungumza juu ya ajali. Picha na Mwandishi wetu

Mganga Mfawidhi Kituo cha Afya Katoro Yohana Kitutu amethibitisha kupokea majeruhi 9 na mwili wa mwanaume mmoja aliyetajwa kuwa ni kondakta wa gari la Kampuni ya Najimnisa.

Kitutu amesema majeruhi 4 walihudumiwa katika Kituo cha Afya Katoro na wengine walipewa rufaa katika Hospitali ya Katoro kwa matibabu zaidi na wote wanaoendelea vizuri huku baadhi ya mashuhuda na manusura wa ajali hiyo wakielezea hali ilivyokuwa.

Sauti ya mganga mfawidhi kituo cha Afya Katoro
Mganga mfawidhi wa kituo cha Afya Katoro Yohanna Kitutu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani). Picha na Mwanadishi wetu
Sauti ya mashuhuda wa ajali