Joy FM
Joy FM
10 September 2026, 18:16

Afya ya mama na mtoto ni jambo muhimu katika maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla miongoni mwa changamoto zinazoweza kuhatarisha maisha ya wajawazito na watoto ni kuchelewa kupata huduma za afya, hasa pale ambapo mgonjwa anahitaji usafiri wa haraka kwenda kituo cha afya.
Na Emmanuel Kamangu
Huduma ya usafiri wa dharula kwa mama mjamzito na mama aliye jifungua yaani M-mama katika halmashauri ya mji wa kasulu imefanikiwa kupunguza vifo vya mama na mtoto karibu kwa asilimia 90.
Akizungumz na redio joy Bw, Augustin Karol ambaye ni Mratibu wa M-Mama katika halmashauri ya mji wa kasulu amebainisha kuwa kwa miaka ya hivi karibuni jumla ya vifo 30 vya mama vitokavyo na uzazi vimekuwa vikiibuliwa tofauti na hivi sasa ambapo kuanzia January mpaka septemba ya mwaka huu 2026 ni vifo viwili pekee ambavyo vimeibuliwa.
Aidha Bw, Karoli amemtaka mama mjamzito kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya unaowataka kujali mda sahihi wa kiliniki ili kuendelea kuhakikisha vifo vya mama na mtoto vinakuwa historia.
Katika hatua nyingine Bw, Karoli ameeleza kuwa uhaba wa magari na miundombinu ya babara mibovu kwa maeneo mengi ya vijijini imekuwa ni moja ya sababu inayopeleka mjamzito kuchelewa kufikishwa katika vituo vya afya hali inayohatarisha usalama wa mama na mtoto.
Hata hivyo Bw, Karoli amewataka wananchi wanapoona hali ya hatari kwa mama mjamzito au mtoto mchanga kutumia namba 115 ambayo itasaidia watoa huduma kufika eneo husika kwa ajili ya msaada wa dharula.