Joy FM
Joy FM
21 August 2026, 16:14

Usimamizi wa miradi na kuikamilisha kwa wakati husaidia kuanza kutoa huduma zilizo bora kwa wananchi
Na Mwandishi wetu
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro amezitaka Halmashauri Mkoani humo kuendelea kuzingatia usimamizi wa miradi na kuikamilisha kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa
Balozi Sirro amesema hayo akiwa wilayani Kibondo katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo ambayo itapitiwa na mbio za mwenge mwezi septemba,2026.

Amesema matarajio ya serikali pamoja na wananchi ni kuona miradi ikitekelezwa katika viwango vinavyotarajiwa na kukamilika kwa wakati
Aidha Balozi Sirro ameipongeza halmashauri ya wilaya ya Kibondo kwa usimamizi wa miradi ulio thabiti kulingana na thamani ya kila mradi.

Naye mkuu wa wilaya ya Kibondo Kanali mstaafu Aggrey Magwaza amesema umeshauri ambao umetolewa na mkuu wa mkoa Balozi Sirro watauzingatia na kuboresha mahali ambapo patakuwa na mapungufu