Joy FM

Wamiliki wa famasi Kasulu wahimizwa kusajili biashara zao

17 July 2026, 11:35

Washiriki wa mafunzo hayo, Picha na Emmanuel Kamangu

Usajili na urasimishaji wa biashara za famasi na maduka ya dawa muhimu ni jambo la msingi katika kuhakikisha upatikanaji wa huduma salama na bora za afya kwa wananchi.

Na Emmanuel Kamangu

Wamiliki wa famasi na maduka ya dawa muhimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu wamehimizwa kusajili na kurasimisha biashara zao kwa mujibu wa sheria  ikiwa ni kuboresha huduma za afya na kuhakikisha  usalama wa wananchi unazingatiwa.

Wito huo umetolewa na  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, CPA Francis Kafuku, wakati akifungua mafunzo endelevu ya utoaji wa huduma za famasi na maduka ya dawa muhimu ambapo amesema  zaidi ya maduka ya dawa 300 hayajasajiliwa  na ambayo yamesajiliwa na kurasimishwa yakiwa maduka ya dawa  33 pekee.

Mkurugenzi mtendaji halmashauri ya wilaya ya kasulu CPA Fransis Kafuku, Picha na Emmanuel Kamangu

CPA Kafuku ameongeza kuwa kutokusajiliwa kwa maduka mengi ya dawa ni kutarisha afya za wananchi wa halmashauri ya wilaya hiyo ikiwemo kudororsha  ukusanyaji  wa  mapato kwa maendeleo ya wananchi.

Aidha  Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Dkt. Mageni Pondamali, amesema mafunzo hayo yamelenga  kuwajengea uwezo wamiliki wa famasi na maduka ya dawa muhimu pamoja na kuwahamasisha kurasimisha biashara zao kisheria kwa kuzingatia kanuni za kiafya ili kutoa huduma kwa ufansi.

Kaimu mganga mkuu halmashauri ya wilaya ya kasulu Pondamali, Picha na Emmanuel Kamangu

Kwa upande wake  Mfamasia wa Wilaya hiyo Bw. Faustin Kasalya, amewataka wamiliki wa maduka ya dawa muhimu kuhakikisha wanauza dawa zilizoidhinishwa kwa mujibu wa sheria ikiwemo kuhakiksha watumishi wanaowaajiri wanakidhi sifa na vigezo vinavyotakiwa .

Baadhi ya  washiriki wa mafunzo hayo mmoja wao akiwa  Bw, Kawambwa Kawambwa ameishauri  Halmashauri  ya wilaya ya kasulu kuimarisha usimamizi wa ufunguaji wa maduka ya dawa ili kuepuka kendesha maduka yao katika mazingira yasiyo kidhi sifa  kwa usalama wa afya za wanchi.

Sauti ya Emmanuel Kamangu