Joy FM
Joy FM
21 April 2026, 10:07

Umuhimu wa familia kushirikiana kuleta maendeleo ni mkubwa sana katika maisha ya kijamii, kiuchumi na hata kirohona familia inapokuwa na mshikamano na ushirikiano, hujenga msingi imara wa mafanikio kwa kila mwanachama
Na Dotto Josephati
Askofu wa Kanisa la FPCT Kibondo ambaye pia ni mchungaji wa kanisa la FPCT Kibondo mjini mchungaji Buhimbi amewataka wanafamilia kufanya mambo yao kwa ushirikiano na mshikamano kwaajili ya maendeleo ya familia ili waweze kutimiza mipango yao ipasavyo.
Ameyasema hayo katika kilele cha wiki mwanamke ambayo ilianza April 13 hadi 19 ambapo amesema
familia ambayo Haina ushirikiano haiwezi kua na mafanikio.

Vile vile mchungaji Buhimbi amewahimiza waumini wa kanisa Hilo kua na moyo wa utoaji Kwa hitaji ili
waweze kubalikiwa na kuongezewa zaidi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wanawake FPCT Jimbo la Kibondo Angesta Mishita ameeleza lengo la
kuwepo Kwa juma Hilo la Wanawake FPCT ambapo amesema juma hili linalengo la kuwakutanisha
wanawake kwaajili ya mafundisho na kufanya matendo ya huruma Kwa wenye uhitaji.

Hali kadhalika katika hitimisho la wiki mwanamke imeambatana na harambee kwaajili ya kutunisha
mfuko wa Wanawake ambayo utawasaidia kuakamilisha ujenzi ya nyumba yao Kwaajili ya shughuli za
Wanawake huku akiekeza namna fedhahiyo itakavyo wasaidia kutekeleza mipango yao