Joy FM

Serikali yaaswa kukamilisha choo zahanati ya Migunga Kasulu

23 April 2026, 14:47

Diwani wa kata ya Kurugongo Mh. Edson Hanyuma halmashauri ya wilaya ya Kasulu, Picha na Hagai Ruyagila

Choo katika zahanati kina umuhimu mkubwa sana, si suala la ziada bali ni hitaji la msingi kwa huduma bora za afya kwani bila choo, mazingira yanakuwa machafu na yanaweza kusababisha kuenea kwa magonjwa ya mlipuko kama kuhara, kipindupindu na maambukizi mengine.

Na Hagai Ruyagila

Diwani wa Kata ya Kurugongo, Halmashauri ya wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma, Mh. Edson Hanyuma, ameiomba serikali kuongeza juhudi katika kukamilisha ujenzi wa choo katika Zahanati ya Migunga, ili kuboresha mazingira ya utoaji huduma za afya kwa wananchi.

Mhe, Hanyuma ametoa ombi hilo wakati akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya kata yake, katika mkutano wa Baraza la madiwani Halmashauri ya wilaya ya Kasulu katika kikao cha robo ya tatu cha mwaka wa fedha 2025/2026.

Amesema kukamilika kwa miundombinu hiyo, hususan choo, kutachangia kwa kiasi kikubwa kuboresha huduma za afya na kupunguza changamoto zinazowakabili wananchi wanapohitaji huduma.

Sauti ya Mh Edson Hanyuma

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kasulu, Mh. Charles Benjamini, ambaye pia aliyekuwa mwenyekiti wa kikao hicho, amesema serikali inatabua umuhimu wa kuboresha miundombinu ya sekta ya afya na imejipanga kuhakikisha ujenzi wa choo hicho unakamilika kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika na huduma bora.

Sauti ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kasulu, Mh. Charles Benjamini
Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kasulu, Mh. Charles Benjamini, Picha na Hagai Ruyagila