Joy FM
Joy FM
15 July 2026, 09:02

Elimu ni msingi muhimu wa maendeleo ya mtu binafsi na taifa kwa ujumla na kupitia elimu, jamii hupata maarifa, ujuzi na maadili yanayochangia maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa, utekelezaji wa miradi ya elimu unahitaji rasilimali nyingi, utaalamu na ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali
Na Hagai Ruyagila
Shirika la Enabel limekabidhi madarasa matatu ya kisasa yanayohamishika (Digitruck) kwa Serikali mkoani Kigoma yenye thamani ya shilingi milioni 600 yakiwa na kompyuta mpakato ili kuwawezesha walimu wa shule za Sekondari kuboresha mbinu za ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi.
Zoezi la kukabidhi madarasa hayo limefanyika katika kata ya Nyansha mjini Kasulu na yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali mkoani Kigoma washirika wa Enabel kutoka Nchini Kenya,Uganda na Rwanda.

Mtaalamu wa kidigitali kutoka shirika la Enabel Walter John amesema mradi huo unalenga kuleta manufaa kwa waalimu na wanafunzi katika shule za sekondari.

Mkurugenzi wa shirika la Enabel nchini Tanzania anayemaliza muda wake Geokint Koenraad amesema madarasa hayo yanayohamishika kwa kitalaamu Digitruck yamewekwa kwenye vituo vya rasilimali za walimu katika kata za Nyasha Halmashauri ya mji Kasulu Kata ya kizazi halmashauri ya wilaya ya Kibondo na kata ya Bitale Halmashauri ya wilaya ya Kigoma.
Mkuu wa mkoa wa Kigoma Balozi Simon Sirro ambaye amewakilishwa na Mkuu wa wilaya ya Kasulu kanali Isaac mwakisu amezindua madarasa na vifaa hivyo nakukabidhi funguo kwa wakurugenzi wa Halmashauri zinazonufaika na mradi huo

Nakueleza kuwa utakuwa na manufaa kwa jamii katika idara mbalimbali huku akisisitiza utunzaji wa vifaa hivyo.

Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya wakurugenzi wa Wilaya ya Kibondo na wilaya ya Kigoma, Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji Kasulu Mwl.Vumilia Simbeye amesema watasimamia vifaa hivyo na kuhakikisha vinaleta manufaa kwa wananchi,waalimu na wanafunzi.
