Joy FM
Joy FM
12 December 2024, 09:21

Meneja wa mamlaka ya udhibiti wa nishati na maji EWURA Kanda ya Magharibi Mhandisi Walter Christopher amewataka wadau wa masuala ya uuzaji wa mafuta kutumia fursa ya kuwekeza katika maeneo ya vijijini ambako kuna uhaba mkubwa wa vituo vya mafuta.
Na Kadislaus Ezekiel – Kasulu
Mamlaka ya udhibiti wa Nishati na Maji EWURA Kanda ya Magharibi inayojumusiha mikoa ya Tabora, Shinyanga, Katavi na Kigoma imeonya uuzaji holela wa mafuta ya vyombo vya moto katika madumu hasa maeneo ya vijijini na kuwa itawachukulia hatua kali za kisheria kutokana na wafanyabiashara kutumia fursa ya uhaba wa vituo vya mafuta kuwekeza maeneo hayo.
Kwa sasa Mkoa mzima wa Kigoma kuna vituo 10 pekee vya mafuta maeneo ya vijijini, hali inayosababisha uwepo wa uhaba mkubwa wa mafuta na kuwalazimu baadhi ya wananchi kufuata mafuta mjini na kuyauza kiholela bila kufuata kanuni na utalatibu.

Meneja EWURA Kanda ya Magharibi Mhandisi Walter Christopher anawataka wafanyabiashara kutumia frusa hiyo kuwekeza vituo vya mafuta kuepusha athari kwa jami na kuondokana na uuzaji huolela.
Mhandisi Christopher ametoa wito huo wakati wa mafunzo kwa wadau wa mafuta Wilayani Kasulu yenye lengo la kuwejengea uwezo wa masuala ya kiudhibiti wadau wa sekta ndogo ya petroli kutoka mkoa wa Kigoma ukijumuisha washiriki kutoka wilaya zote sita za Kigoma, Kasulu, Kibondo, Kakonko, Buhigwe na Uvinza.
Kwa upande wao, baadhi ya wauzaji wa mafuta na wadau, wametoa maoni yao katika kufanikisha suala hilo na kuwa ni frasa katika kukuza uchumi.
